Jan 19, 2014

Tajiri wa kichina Wang Jianlin kuifanya Southampton timu tajiri zaidi ligi kuu ya Uingereza

Posted at  1/19/2014  |  in  Michezo


Tajiri kuliko wote nchini China Wang Jianlin, ajiandaa kuweka mezani kitita ili kuinyakua Southampton.

Ikiwa atafanikiwa basi itamaanisha Nicola Cortese atarudi Southampton kama mwenyekiti wa klabu hiyo.

Inasemekana meneja wa klabu hiyo Mauricio Pachettino, anaijua nia ya Billionea huyo kiongozi wa kampuni ya uwekezaji ijulikanayo kwa jina la Wanda.

Kampuni ya Wanda ina utajiri wa Billiona 175, nusu ya utajiri huo ukiwa ya Wang Jianlin.

Jianlin anadhamiria kuingia katika ligi kuu ya Uingereza ili kuitangaza zaidi kampuni yao ya Wanda, kwa kumwanga mezani paundi millioni 175; ambayo itamfanya mmiliki wa sasa Liebherr asiwe na ujanja mwingine zaidi ya kulikubali donge hilo.

Kwa mujibu wa gazeti la Uingereza la Daily Mirror, mazungumzo ya dili hilo yameshaanza na yanaelekea kufanikiwa.

Iwapo dili hilo litakamilika litaifanya Southampton kuwa klabu tajiri zaidi katika ligi kuu ya Uingereza.

Share this post

About Naveed Iqbal

Nulla sagittis convallis arcu. Sed sed nunc. Curabitur consequat. Quisque metus enim venenatis fermentum mollis. Duis vulputate elit in elit. Follow him on Google+.

0 comments:

About-Privacy Policy-Contact us
Copyright © 2013 mchambuzi@habari online. Blogger Template by Bloggertheme9
Proudly Powered by Blogger.
back to top