Mar 3, 2014

Hatuwa ya Urusi kuwatuma wanajeshi wake katika mji wa Crimea yazua wasiwasi nchini Ukraine

Posted at  3/03/2014  |  in  Habari

Malori ya kijeshi ya Urusi katika mji wa Crimea

Waziri Mkuu wa Ukraine Arseniy Yatsenyuk anasema taifa lake liko katika hali ya hatari na ameishtumu Urusi kutangaza vita dhidi ya nchi yake. Wanajeshi wa Urusi kwa sasa wanapiga kambi katika mji wa Crimea ambao upo mpakani mwa mataifa hayo mawili na maakazi ya wananchi wa Mataifa yote mawili.

Yatsenyuk anamtaka rais Putin kuamuru wanajeshi wake kurejea katika kambi zao na kuheshimu maafikiano ya Kimataifa kuhusu eneo hilo la Crimea.
Moscow inasema kuwa jeshi lake linawalinda raia wake katika mji huo ambao tayari majengo kadhaa ya serikali yamesimikwa na Bendera ya Urusi.
Viongozi wa Mataifa ya Magharibi wakiongozwa na rais wa Marekani Barrack Obama wameishtumu Urusi kuvamia Ukraine kijeshi na kutishia kusita uhusiano wao na Moscow ikiwa haitawaiondoa wanajeshi wake.
Hayo yanajiri wakati Urusi ikiendelea kutishia kuingilia kijeshi nchini Ukraine ambapo inaweza kuzuia mzozo mkubwa wa kimataifa ambao itakuwa ni hatari sana kuwahi kutokea tangu kuvunjika kwa muungano wa mataifa ya kikoministi.
Mataifa ya magharibi yanaendeleza shinikizo dhidi ya hatuwa ya Urusi kupeleka vikosi katika ardhi ya Ukraine ambayo itakuwa ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Mataifa hayo yanatishia pia kuiwekea vikwazo Urusi ambavyo miongoni ni kuitenga zaidi.
Vladimir Poutine bado anaendelea kuzua hali ya sintofahamu kufuatia nia yake, lakini katika mawasiliano kwa njia ya sim na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel, Poutine alikubali kuundwa kwa tume maalum itayo anzisha mazungumzo ya kisiasa nchini Ukraine.

Share this post

About Naveed Iqbal

Nulla sagittis convallis arcu. Sed sed nunc. Curabitur consequat. Quisque metus enim venenatis fermentum mollis. Duis vulputate elit in elit. Follow him on Google+.

0 comments:

About-Privacy Policy-Contact us
Copyright © 2013 mchambuzi@habari online. Blogger Template by Bloggertheme9
Proudly Powered by Blogger.
back to top