• HABARI MPYA

    Obama na Putin wajadiliana kuhusu Ukraine

  • HABARI MPYA

    Jack Wilshere nje wiki sita

  • MAKALA

    Cancer in relation to Herat Attack

  • MAKALA

    Diabetes Remedy

  • Mar 18, 2014

    dreamteam12312412412

    Kwa maoni ya wadau wengi wa soka na mashabiki nguli wa Manchester, hiki ndio kikosi bora cha muda wote wa Ferguson akiwa Manchester United.

    Tengeneza kikosi chako bora katika enzi za Fergie, Weka maoni yako hapa chini

    Kikosi bora cha Manchester katika enzi za sir Alex Ferguson hiki hapa

    Posted at  3/18/2014  |  in    |  Read More»

    dreamteam12312412412

    Kwa maoni ya wadau wengi wa soka na mashabiki nguli wa Manchester, hiki ndio kikosi bora cha muda wote wa Ferguson akiwa Manchester United.

    Tengeneza kikosi chako bora katika enzi za Fergie, Weka maoni yako hapa chini

    Mar 9, 2014

    Wenger v Mourinho

    Kati ya michezo ya ligi kuu ya Uingereza isiyopendwa na kocha Arsene Wenger ni dhidi ya Chelsea ya Mourinho. Wakiwa mahasimu wakubwa, Bosi Arsene Wenger anahofu huenda Morinho akaifanya siku yake ikajawa na majonzi. Siku za hivi karibuni Morinho amaemwelezea Wenger kama kocha mwenye mafanikio ya kufeli zaidi katika ligi kuu ya England. Morinho amesema kwamba Wenger anapoteza muda kwa kuiga mchezo wa Barcelona usiowezekana katika mazingira ya Uingereza. Wenger atafikisha mchezo wa 1000 akiwa na Arsenal katika mchezo dhidi ya Chelsea. Kwa sasa Arsenal iko nafasi ya tatu nyuma ya Chesea na Liverpool. Jana jumamosi ilifanikiwa kuelekea nusu fainali ya kombe la FA baada ya kuibwaga Everton mabao 4 - 1.

    Wenger kucheza mchezo wake wa 1000 na Jose Mourinho English Premium League

    Posted at  3/09/2014  |  in  Michezo  |  Read More»

    Wenger v Mourinho

    Kati ya michezo ya ligi kuu ya Uingereza isiyopendwa na kocha Arsene Wenger ni dhidi ya Chelsea ya Mourinho. Wakiwa mahasimu wakubwa, Bosi Arsene Wenger anahofu huenda Morinho akaifanya siku yake ikajawa na majonzi. Siku za hivi karibuni Morinho amaemwelezea Wenger kama kocha mwenye mafanikio ya kufeli zaidi katika ligi kuu ya England. Morinho amesema kwamba Wenger anapoteza muda kwa kuiga mchezo wa Barcelona usiowezekana katika mazingira ya Uingereza. Wenger atafikisha mchezo wa 1000 akiwa na Arsenal katika mchezo dhidi ya Chelsea. Kwa sasa Arsenal iko nafasi ya tatu nyuma ya Chesea na Liverpool. Jana jumamosi ilifanikiwa kuelekea nusu fainali ya kombe la FA baada ya kuibwaga Everton mabao 4 - 1.

    Mar 8, 2014

    Mchezaji wa Arsenal Mikel Arteta

    Magoli manne yametosha kuipeleka Arsenal nusu fainali ya FA itakayochezewa katika uwanja wa Wembley. Ikiwa inacheza na Everton mchezo ulionekana kuwa mgumu kwa Arsenal katika kipindi cha kwanza, japo mambo yalibadilika kipindi cha pili baada ya Rosicky na Giroud  kuchukua nafasi za Chamberlain na Sanogo. Arsenal ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Ozil kabla ya Lukaku kusawazisha katika kipindi cha kwanza. Dakika ya 70 Arsenal ilipata bao la pili kupitia kwa Arteta kwa mkwaju wa Penalt.
    Dakika 10 za mwisho Giroud alipachika wavuni magoli 2 na mechi ikaisha ubao ukisomeka 4 - 1.

    Kwa habari zaidi tembelea:-

    Arsenal yaelekea Wembley

    Posted at  3/08/2014  |  in  Michezo  |  Read More»

    Mchezaji wa Arsenal Mikel Arteta

    Magoli manne yametosha kuipeleka Arsenal nusu fainali ya FA itakayochezewa katika uwanja wa Wembley. Ikiwa inacheza na Everton mchezo ulionekana kuwa mgumu kwa Arsenal katika kipindi cha kwanza, japo mambo yalibadilika kipindi cha pili baada ya Rosicky na Giroud  kuchukua nafasi za Chamberlain na Sanogo. Arsenal ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Ozil kabla ya Lukaku kusawazisha katika kipindi cha kwanza. Dakika ya 70 Arsenal ilipata bao la pili kupitia kwa Arteta kwa mkwaju wa Penalt.
    Dakika 10 za mwisho Giroud alipachika wavuni magoli 2 na mechi ikaisha ubao ukisomeka 4 - 1.

    Kwa habari zaidi tembelea:-

    Paul Kagame;Rais wa Rwanda

    Afrika ya kusini imewaondoa wanadiplomasia watatu raia wa Rwanda ikiwahusisha na shambulizi dhdidi ya makazi ya kiongozi wa zamani wa Rwanda Kayumba Nyamwasa.
    Taarifa zinabainisha kuwa Rwanda nayo imeamuru kuondolewa kwa wajumbe sita wa Afrika ya kusini .
    Hatua hizo zinakuja baada ya watu wenye silaha kushambulia makazi ya Kayumba Nyamwasa aliyewahi kushika wadhifa wa juu katika serikali ya Rwanda.
    Hata hivyo wakati shambulizi hilo mkosoajii wa raisi Kagame Kayumba Nyamwasa hakuwepo nyumbani.
    Generali Nyamwasa ameponea chupuchupu majaribio mawili ya kumuua ambapo mnamo mwaka 2010 alipigwa risasi na kujeruhiwa tukio ambalo Rwanda ilikanusha kuhusika

    wanadiplomasia wa Kinyarwanda watimuliwa Afrika ya Kusini

    Posted at  3/08/2014  |  in  Habari  |  Read More»

    Paul Kagame;Rais wa Rwanda

    Afrika ya kusini imewaondoa wanadiplomasia watatu raia wa Rwanda ikiwahusisha na shambulizi dhdidi ya makazi ya kiongozi wa zamani wa Rwanda Kayumba Nyamwasa.
    Taarifa zinabainisha kuwa Rwanda nayo imeamuru kuondolewa kwa wajumbe sita wa Afrika ya kusini .
    Hatua hizo zinakuja baada ya watu wenye silaha kushambulia makazi ya Kayumba Nyamwasa aliyewahi kushika wadhifa wa juu katika serikali ya Rwanda.
    Hata hivyo wakati shambulizi hilo mkosoajii wa raisi Kagame Kayumba Nyamwasa hakuwepo nyumbani.
    Generali Nyamwasa ameponea chupuchupu majaribio mawili ya kumuua ambapo mnamo mwaka 2010 alipigwa risasi na kujeruhiwa tukio ambalo Rwanda ilikanusha kuhusika

    Mar 6, 2014

    Jack Wilshere

    Mchezaji wa kiungo cha kati wa Arsenal Jack Wilshere atakosa kucheza wiki sita baada ya kupata jeraha la mguu katika mechi aliyochezea England hapo juzi iliposhinda Denmark bao moja kwa bila. Kwa sababu hiyo atakosa mchuano wa FA wa robo fainali hapo kesho dhidi ya Everton na Jumanne ijayo atatazama tu timu yake ikicheza na Bayern Munich katika kombe la kilabu bingwa barani ulaya.
    Si hayo tu atakosa mechi nne muhimu za ligii ya England kati ya Chelsea, Manchester City, Swansea na Tottenham ambazo zinacheza mwezi huu.

    Jack Wilshere nje wiki sita

    Posted at  3/06/2014  |  in  Michezo  |  Read More»

    Jack Wilshere

    Mchezaji wa kiungo cha kati wa Arsenal Jack Wilshere atakosa kucheza wiki sita baada ya kupata jeraha la mguu katika mechi aliyochezea England hapo juzi iliposhinda Denmark bao moja kwa bila. Kwa sababu hiyo atakosa mchuano wa FA wa robo fainali hapo kesho dhidi ya Everton na Jumanne ijayo atatazama tu timu yake ikicheza na Bayern Munich katika kombe la kilabu bingwa barani ulaya.
    Si hayo tu atakosa mechi nne muhimu za ligii ya England kati ya Chelsea, Manchester City, Swansea na Tottenham ambazo zinacheza mwezi huu.

    Rais Obama na Putin

    Rais Obama amefanya mazungumzo zaidi ya kina na rais wa Urusi Vladmir Putin akisistiza kuwa vitendo vya nchi yake katika jimbo la Crimea ni ukiukaji wa mipaka na uhuru wa taifa la Ukraine.
    Wakati wa mazungumzo yao ya pili kupitia njia ya simu katika kipindi cha siku sita zilizopita, bwana Obama amependekeza njia ya kusuluhisha mzozo huo kidiplomasia inayojumuisha Urusi kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo la Crimea. Bwana Putin amesema uhusiano kati ya Moscow na Washington haufai kutatizika kutokana na mzozo wa Ukraine.
    Awali bwana alisema kuwa kura ya maoni iliyopendekezwa kuhusu jimbo la Crimea kujiunga na Moscow inakiuka sheria ya kimataifa na sharti ijumuishe serikali ya Kiev iwapo itaandaliwa.
    Akizungumza baada ya mkutano mwingine wa Baraza la Usalama uliofanyika faraghani, balozi wa Uingireza katika umoja wa mataifa , Mark Lyall Grant, amesema haiwezekani muafaka kupatikana katika baraza hilo kuhusu mzozo huo.
    "Nadhani hakuna dalili kwamba kutakuwa na mwafaka katika baraza la usalama katika kipindi cha siku chache zijazo. Kama ulivyosikia kutoka kwa wengine, kuna mashauri yanayoendelea kati ya wanadiplomasia kwenye mikutano mbali mbali Ulaya. Mashauri hayo yataendelea,'' amesema bwana Grant.
    ''Pengine kiwango fulani cha makubaliano kitaafikiwa ili kutuliza mgogoro huu na kisha baraza la usalama pengine litapata suluhu. Lakini hatujafutilia mbali mpango wa kuwasilisha azimio mbele ya Baraza la Usalama wakati wowote na tunafuatilia hali ya mambo kwa karibu tukitarajia baraza la Usalama likutane tena katika siku chache zijazo ikitegemea kitakachotokea mashinani."
    Mzozo huo wa Ukraine umechochea wanasiasa pamoja na wageni wengine mashuhuri kususia mashindano ya Olimpiki ya wanariadha walemavu nchini Urusi. Marekani imeondoa ujumbe wake katika michezo hiyo na mawaziri wa Uingereza hawatakuwepo sawia na wenzao kutoka mataifa mengine ya Ulaya.
    Habari na BBC SWAHILI

    Obama na Putin wajadiliana kuhusu Ukraine

    Posted at  3/06/2014  |  in  Habari  |  Read More»

    Rais Obama na Putin

    Rais Obama amefanya mazungumzo zaidi ya kina na rais wa Urusi Vladmir Putin akisistiza kuwa vitendo vya nchi yake katika jimbo la Crimea ni ukiukaji wa mipaka na uhuru wa taifa la Ukraine.
    Wakati wa mazungumzo yao ya pili kupitia njia ya simu katika kipindi cha siku sita zilizopita, bwana Obama amependekeza njia ya kusuluhisha mzozo huo kidiplomasia inayojumuisha Urusi kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo la Crimea. Bwana Putin amesema uhusiano kati ya Moscow na Washington haufai kutatizika kutokana na mzozo wa Ukraine.
    Awali bwana alisema kuwa kura ya maoni iliyopendekezwa kuhusu jimbo la Crimea kujiunga na Moscow inakiuka sheria ya kimataifa na sharti ijumuishe serikali ya Kiev iwapo itaandaliwa.
    Akizungumza baada ya mkutano mwingine wa Baraza la Usalama uliofanyika faraghani, balozi wa Uingireza katika umoja wa mataifa , Mark Lyall Grant, amesema haiwezekani muafaka kupatikana katika baraza hilo kuhusu mzozo huo.
    "Nadhani hakuna dalili kwamba kutakuwa na mwafaka katika baraza la usalama katika kipindi cha siku chache zijazo. Kama ulivyosikia kutoka kwa wengine, kuna mashauri yanayoendelea kati ya wanadiplomasia kwenye mikutano mbali mbali Ulaya. Mashauri hayo yataendelea,'' amesema bwana Grant.
    ''Pengine kiwango fulani cha makubaliano kitaafikiwa ili kutuliza mgogoro huu na kisha baraza la usalama pengine litapata suluhu. Lakini hatujafutilia mbali mpango wa kuwasilisha azimio mbele ya Baraza la Usalama wakati wowote na tunafuatilia hali ya mambo kwa karibu tukitarajia baraza la Usalama likutane tena katika siku chache zijazo ikitegemea kitakachotokea mashinani."
    Mzozo huo wa Ukraine umechochea wanasiasa pamoja na wageni wengine mashuhuri kususia mashindano ya Olimpiki ya wanariadha walemavu nchini Urusi. Marekani imeondoa ujumbe wake katika michezo hiyo na mawaziri wa Uingereza hawatakuwepo sawia na wenzao kutoka mataifa mengine ya Ulaya.
    Habari na BBC SWAHILI

    Mar 5, 2014

    Carles Puyol

    Nahodha wa klabu ya Barcelona Carles Puyol ametangaza atawahama mabingwa hao wa Hispania mwishoni mwa msimu huu.
    Puyol mwenye umri wa miaka 35 aliibukia kutoka vikosi vya vijana wa Barcelona na kujiunga na kikosi kikuu mwaka 1999.
    Amewachezea mabingwa watetezi wa La Liga takriban mara 400.
    Ameshinda vikombe sita vya ubingwa wa Ligi,vikombe vitatu vya klabu bingwa ya Ulaya,vikombe viwili vya shirikisho la kandanda la Uhispania pamoja na vikombe vya super cup vya klabu za ulaya na Uhispania.
    Pia amekua mchezaj muhimu katika nyanja ya kimataifa akiisaidia Hispania kunyakua ubingwa wa bara la Ulaya mwaka 2008 na kombe la dunia miaka miwili badae.
    Hata hivyo amekua akisumbuliwa na magoti katika miaka ya hivi karibuni na hakuweza kushiriki katika michuano ya kombe la mataifa ya Ulaya mwaka 2012.
    Msimu huu ameichezea Barcelona mara 12 tu.
    Puyol, ambae ameiwakilisha Hispania mara 100,alicheza mechi yake ya mwisho dhidi ya Uruguay, Februari 2013.
    Amesema angependa kupumzika baada ya kuondoka Barcelona. "sijui ntakachofanya baada ya Juni 30 lakini nina hakika nitapumzika" akaongeza.
    "nitaitisha mkutano na waandishi habari mwishoni mwa msimu huu ili niwaage baada ya kuichezea klabu hii kwa muda wa miaka 19 ," alisema Puyol

    Carles Puyol Kutimka Barcelona

    Posted at  3/05/2014  |  in  Michezo  |  Read More»

    Carles Puyol

    Nahodha wa klabu ya Barcelona Carles Puyol ametangaza atawahama mabingwa hao wa Hispania mwishoni mwa msimu huu.
    Puyol mwenye umri wa miaka 35 aliibukia kutoka vikosi vya vijana wa Barcelona na kujiunga na kikosi kikuu mwaka 1999.
    Amewachezea mabingwa watetezi wa La Liga takriban mara 400.
    Ameshinda vikombe sita vya ubingwa wa Ligi,vikombe vitatu vya klabu bingwa ya Ulaya,vikombe viwili vya shirikisho la kandanda la Uhispania pamoja na vikombe vya super cup vya klabu za ulaya na Uhispania.
    Pia amekua mchezaj muhimu katika nyanja ya kimataifa akiisaidia Hispania kunyakua ubingwa wa bara la Ulaya mwaka 2008 na kombe la dunia miaka miwili badae.
    Hata hivyo amekua akisumbuliwa na magoti katika miaka ya hivi karibuni na hakuweza kushiriki katika michuano ya kombe la mataifa ya Ulaya mwaka 2012.
    Msimu huu ameichezea Barcelona mara 12 tu.
    Puyol, ambae ameiwakilisha Hispania mara 100,alicheza mechi yake ya mwisho dhidi ya Uruguay, Februari 2013.
    Amesema angependa kupumzika baada ya kuondoka Barcelona. "sijui ntakachofanya baada ya Juni 30 lakini nina hakika nitapumzika" akaongeza.
    "nitaitisha mkutano na waandishi habari mwishoni mwa msimu huu ili niwaage baada ya kuichezea klabu hii kwa muda wa miaka 19 ," alisema Puyol

    Mar 3, 2014

    Nyoka ammeza mamba mzimamzima
    Chatu akipigana na mamba mwenye urefu wa futi sita kaskazini mwa mlima Isa ulioko Outback Queensland

    Nyoka ammeza mamba mzimamzima
    Mamba alibanwa na kufa papo hapo

    Nyoka ammeza mamba mzimamzima
    Chatu akimmeza mamba baada ya kumuuwa

    Nyoka ammeza mamba mzimamzima

    Angalia picha za ajabu: Nyoka apigana na mamba na kummeza

    Posted at  3/03/2014  |  in  Makala  |  Read More»

    Nyoka ammeza mamba mzimamzima
    Chatu akipigana na mamba mwenye urefu wa futi sita kaskazini mwa mlima Isa ulioko Outback Queensland

    Nyoka ammeza mamba mzimamzima
    Mamba alibanwa na kufa papo hapo

    Nyoka ammeza mamba mzimamzima
    Chatu akimmeza mamba baada ya kumuuwa

    Nyoka ammeza mamba mzimamzima

    Malori ya kijeshi ya Urusi katika mji wa Crimea

    Waziri Mkuu wa Ukraine Arseniy Yatsenyuk anasema taifa lake liko katika hali ya hatari na ameishtumu Urusi kutangaza vita dhidi ya nchi yake. Wanajeshi wa Urusi kwa sasa wanapiga kambi katika mji wa Crimea ambao upo mpakani mwa mataifa hayo mawili na maakazi ya wananchi wa Mataifa yote mawili.

    Yatsenyuk anamtaka rais Putin kuamuru wanajeshi wake kurejea katika kambi zao na kuheshimu maafikiano ya Kimataifa kuhusu eneo hilo la Crimea.
    Moscow inasema kuwa jeshi lake linawalinda raia wake katika mji huo ambao tayari majengo kadhaa ya serikali yamesimikwa na Bendera ya Urusi.
    Viongozi wa Mataifa ya Magharibi wakiongozwa na rais wa Marekani Barrack Obama wameishtumu Urusi kuvamia Ukraine kijeshi na kutishia kusita uhusiano wao na Moscow ikiwa haitawaiondoa wanajeshi wake.
    Hayo yanajiri wakati Urusi ikiendelea kutishia kuingilia kijeshi nchini Ukraine ambapo inaweza kuzuia mzozo mkubwa wa kimataifa ambao itakuwa ni hatari sana kuwahi kutokea tangu kuvunjika kwa muungano wa mataifa ya kikoministi.
    Mataifa ya magharibi yanaendeleza shinikizo dhidi ya hatuwa ya Urusi kupeleka vikosi katika ardhi ya Ukraine ambayo itakuwa ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Mataifa hayo yanatishia pia kuiwekea vikwazo Urusi ambavyo miongoni ni kuitenga zaidi.
    Vladimir Poutine bado anaendelea kuzua hali ya sintofahamu kufuatia nia yake, lakini katika mawasiliano kwa njia ya sim na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel, Poutine alikubali kuundwa kwa tume maalum itayo anzisha mazungumzo ya kisiasa nchini Ukraine.

    Hatuwa ya Urusi kuwatuma wanajeshi wake katika mji wa Crimea yazua wasiwasi nchini Ukraine

    Posted at  3/03/2014  |  in  Habari  |  Read More»

    Malori ya kijeshi ya Urusi katika mji wa Crimea

    Waziri Mkuu wa Ukraine Arseniy Yatsenyuk anasema taifa lake liko katika hali ya hatari na ameishtumu Urusi kutangaza vita dhidi ya nchi yake. Wanajeshi wa Urusi kwa sasa wanapiga kambi katika mji wa Crimea ambao upo mpakani mwa mataifa hayo mawili na maakazi ya wananchi wa Mataifa yote mawili.

    Yatsenyuk anamtaka rais Putin kuamuru wanajeshi wake kurejea katika kambi zao na kuheshimu maafikiano ya Kimataifa kuhusu eneo hilo la Crimea.
    Moscow inasema kuwa jeshi lake linawalinda raia wake katika mji huo ambao tayari majengo kadhaa ya serikali yamesimikwa na Bendera ya Urusi.
    Viongozi wa Mataifa ya Magharibi wakiongozwa na rais wa Marekani Barrack Obama wameishtumu Urusi kuvamia Ukraine kijeshi na kutishia kusita uhusiano wao na Moscow ikiwa haitawaiondoa wanajeshi wake.
    Hayo yanajiri wakati Urusi ikiendelea kutishia kuingilia kijeshi nchini Ukraine ambapo inaweza kuzuia mzozo mkubwa wa kimataifa ambao itakuwa ni hatari sana kuwahi kutokea tangu kuvunjika kwa muungano wa mataifa ya kikoministi.
    Mataifa ya magharibi yanaendeleza shinikizo dhidi ya hatuwa ya Urusi kupeleka vikosi katika ardhi ya Ukraine ambayo itakuwa ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Mataifa hayo yanatishia pia kuiwekea vikwazo Urusi ambavyo miongoni ni kuitenga zaidi.
    Vladimir Poutine bado anaendelea kuzua hali ya sintofahamu kufuatia nia yake, lakini katika mawasiliano kwa njia ya sim na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel, Poutine alikubali kuundwa kwa tume maalum itayo anzisha mazungumzo ya kisiasa nchini Ukraine.

    Yoweri Kaguta Museveni rais wa Uganda

    Serikali ya Uganda imesema Bajeti yake ya mwaka huu wa 2014 haitaathirika ikiwa Mataifa ya Magharibi yatasitisha misaada ya kifedha kutokana na hatua ya rais Yoweri Museveni kusaini mswada unaopiga marufuku mapenzi ya jinsia moja nchini humo. Kampala inasema haitakuwa mara ya kwanza kwa Mataifa hayo kusitisha misaada.

    Uganda: bajeti ya mwaka huu 2014 haitaathirika iwapo mataifa ya magharibi yatasitisha msaada

    Posted at  3/03/2014  |  in  Habari  |  Read More»

    Yoweri Kaguta Museveni rais wa Uganda

    Serikali ya Uganda imesema Bajeti yake ya mwaka huu wa 2014 haitaathirika ikiwa Mataifa ya Magharibi yatasitisha misaada ya kifedha kutokana na hatua ya rais Yoweri Museveni kusaini mswada unaopiga marufuku mapenzi ya jinsia moja nchini humo. Kampala inasema haitakuwa mara ya kwanza kwa Mataifa hayo kusitisha misaada.

    About-Privacy Policy-Contact us
    Copyright © 2013 mchambuzi@habari online. Blogger Template by Bloggertheme9
    Proudly Powered by Blogger.
    back to top