Feb 3, 2014

Kenya:Polisi wavamia msikiti Mombasa; watatu wauwawa

Posted at  2/03/2014  |  in  Habari

Polisi Wavamia msikiti Mombasa

Watu 3 akiwemo polisi wameuawa na wengine kadha kujeruhiwa kwenye ghasia katika mji wa Mombasa, Kenya, baada ya polisi kuvamia msikiti unaosemekana kutoa mafunzi ya itikadi kali za dini ya kiisilamu
Polisi walitumia moshi wa kutoza machozi na risasi za raba dhidi ya waandamanaji na kuwakamata watu 100.
Viongozi wa mombasa wamelaani kitendo cha polisi wakisema kuwa ni kinyume na sheria.
Mashekhe wawili ambao wakihubiri katika msikiti wa Masjid Mussa walipigwa risasi na kuuliwa na watu wasiojulikana katika miezi ya karibuni.
Polisi wa Kenya wameuhusisha msikiti huo na kuajiri wapiganaji wa kundi la wapiganaji Waislamu wa Somalia, Al Shabaab, ambalo mwaka jana lilishambulia jumba la maduka la Westgate mjini Nairobi.

Share this post

About Naveed Iqbal

Nulla sagittis convallis arcu. Sed sed nunc. Curabitur consequat. Quisque metus enim venenatis fermentum mollis. Duis vulputate elit in elit. Follow him on Google+.

0 comments:

About-Privacy Policy-Contact us
Copyright © 2013 mchambuzi@habari online. Blogger Template by Bloggertheme9
Proudly Powered by Blogger.
back to top