Dec 29, 2013

TOM HUDDLESTONE ANYOA NYWELE ZAKE BAADA YA KUMALIZA UKAME WA MABAO

Posted at  12/29/2013  |  in  Michezo

mchezaji wa hull city tom huddlestone
kiungo wa Hull City Tom Huddleston akinyolewa nywele na daktari wa timu Rob Price baada ya kuifungia timu yake goli

Kiungo wa Hull City  Tom Huddlestone hatimaye alivunja ukame wake wa kupachika mabao, na kuamua kukata nyele zake.
Mchezaji huyo wa zamani wa Spurs alikuwa hajaziona nyavu kwa zaidi ya mwaka mpaka jana katika mchezo dhidi ya  Fulham, kutokana na ukame huo aliahidi kutonyoa nywele zake mpaka pale atakapofunga bao.

Baada ya kufunga goli jana katika uwanja wa KC alikimbia moja kwa moja kwenye benchi la ufundi na kumwomba daktari wa timu Rob Price amnyoe nyele kidogo kutumia mkasi wa kufanyia upasuajia.
Hata hivyo goli hilo lilikuwa kama zawadi yake ya siku ya kuzaliwa kwani jana alifikisha miaka 26.
Hull iliipiga Fulham magoli 6 - 0.
mchezaji wa hull city tom huddlestone
Wachezaji wa timu ya Hull City wakishangilia goli lililopachikwa na Tom Huddlestone 



Share this post

About Naveed Iqbal

Nulla sagittis convallis arcu. Sed sed nunc. Curabitur consequat. Quisque metus enim venenatis fermentum mollis. Duis vulputate elit in elit. Follow him on Google+.

0 comments:

About-Privacy Policy-Contact us
Copyright © 2013 mchambuzi@habari online. Blogger Template by Bloggertheme9
Proudly Powered by Blogger.
back to top